IJUE DINI YA KIISLAM
Swali: "Uislamu ni nini ?
Neno Uislam limetokana na neno Islam ambalo kiini chake ni (SLM) au Salam, ambayo maana yake ni amani au kujisalimisha. Kwa hiyo kimaana, neno Uislamu (Islam) ni kule kupatikana amani ya ndani na nje kunakotokana na kujisalimisha kwa Muumba (s.w.). Kwa maana nyingine Uislamu ni kufuata mwenendo mwema unaozingatia maelekezo ya Muumba au kwa maana ingine
"Uislamu" maana yake "anayetii Mwenyezi Mungu na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mungu wa pekee wa kweli na kwamba Muhammad alikuwa Mtume wa Mwenyezi Mungu na Qur'an ni kitabu takatifu cha Uislamu.
Imani ya dini ya Uislam una nguzo kuu tano, nazo ni:-
1. Shahada: "Hapana Mola ( Mwenyezi Mungu ) apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa ALLAH na Muhammad ( S.A.W ) ni Mtume wa Mungu."
2. Swala:. Kuswali swala tano Alfajiri ( saa kumi na moja Alfajiri ) ,Adhuhuri ( saa saba mchana ), Alasiri ( saa Kumi jioni ) , Magharibi ( saa kumi na mbili jioni ) na Insha ( saa mbili usiku )
3. Kutoa Zaka: mtu lazima atoe kwa ajili ya masikini, asilimia fulani ya pato lake kulingana na anavyopata Mali zake kwa mwaka vile wote hutoka kwa Mwenyezi Mungu.
4. kufunga Ramadhani: kando ya kufunga mara kwa mara, Waislamu wote lazima wafunge wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani (mwezi wa tisa wa kalenda ya Kiislamu), siku ishirini na tisa (29) kama mwezi ukiindama na kama haujaandama ni lazima kumalizia siku thelathini (30).
5. Hija: Kwenda kuhiji Makka kwa mwenye uwezo (Makkah) angalau mara moja katika maisha ya mtu (wakati wa mwezi wa kumi na mbili katika kalenda ya Kiislamu).
Uislam una nguzo sita za Imani, nazo ni:-
1. Kumuamini ALLAH ( Mwenyezi Mungu ni muweza wa yote )
2. Kuamini Malaika wa ALLAH
3. Kuviamini vitabu Takatifu vya ALLAH Qurani, Injili na Torati
4. Kuamini Mitume wote wa ALLAH
5. Kuamini siku ya mwisho ( Kiama)
6. Kuamini Qadari ya ALLAH ( ya kheri au ya shari ) kuwa inatoka kwa ALLAH
NA NGUZO YA TATU NA YA MWISHO NI IHSANI.
1.Kumuabudu Allah

Huu kwa muhtasari ndio Uislamu, dini na mfumo sahihi na kamili wa maisha kwa wanadamu wote waliochaguliwa na Allah Mola Muumba wao: |………LEO NIMEKUKAMILISHENI DINI YENU NA KUKUTIMIZIENI NEEMA YANGU NA NIMEKUPENDELEENI UISLAMU UWE DINI YENU ………….” (5:3) elewa na ufahamu kwamba kuishi nje ya dini hii ni kulikana umbile lako kwani UISLAMU NI HAKI YAKO YA KUZALIWA uliyopewa hadiya (zawadi) na Mola Muumba wako.


















